Wakala wa Vipimo ni Taasisi (Wakala) ya Serikali iliyochini ya Wizara ya Viwanda na Biashara. Taasisi hii iliundwa kwa mujibu wa Sheria ya Wakala za Serikali Sura Na. 245, mapitio ya mwaka 2002. Wakala wa Vipimo ilianzishwa rasmi tarehe 13 Mei, 2002 kwa amri ya Serikali Na. 194 (Government Order No. 194) na kutangazwa tarehe 17 Mei, 2002. Wakala wa Vipimo ina jukumu la kumlinda mlaji kwa kuhakiki vipimo vyote vinavyotumika katika sekta za Biashara, Afya, Usalama na Mazingira.
MHIFADHI WANYAMAPORI DARAJA LA II – NAFASI 31
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii.
7.1 MAJUKUMU YA KAZI
• Kufanya doria ndani na nje ya maeneo ya hifadhi
• Kudhibiti vitendo vya ujangili nje na ndani ya hifadhi
• kusimamia uwindaji wa kitalii na utalii wa picha
• kulinda Nyara za Serikali
• Kusimamia usafirishaji wa wanyamapori na nyara nje na ndani ya Nchi
• Kusimamia matumizi ya magari ya doria
• Kukagua wanyamapori kwenye mashamba na mazizi ya wanyamapori na kutunza takwimu zao
• Kuratibu uingiaji wa wageni katika Mapori ya Akiba
• Kudhibiti moto katika hifadhi
• Kukusanya na kutunza vielelezo vya ushahidi na kutoa ushahidi Mahakamani
• Kukusanya takwimu za wanyama na mimea kwenye hifadhi
• Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa zinazoendana na taaluma yake
7.2 SIFA ZA MWOMBAJI
• Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha IV au kidato cha VI wenye Stashahada ya Uhifadhi Wanyamapori (Diploma in Wildlife Management) kutoka Chuo cha Usimamizi Wanyamapori Mweka au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.
7.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.
MHIFADHI WANYAMAPORI DARAJA LA II – NAFASI 31
Nafasi hizi ni kwa ajili ya Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii.
7.1 MAJUKUMU YA KAZI
• Kufanya doria ndani na nje ya maeneo ya hifadhi
• Kudhibiti vitendo vya ujangili nje na ndani ya hifadhi
• kusimamia uwindaji wa kitalii na utalii wa picha
• kulinda Nyara za Serikali
• Kusimamia usafirishaji wa wanyamapori na nyara nje na ndani ya Nchi
• Kusimamia matumizi ya magari ya doria
• Kukagua wanyamapori kwenye mashamba na mazizi ya wanyamapori na kutunza takwimu zao
• Kuratibu uingiaji wa wageni katika Mapori ya Akiba
• Kudhibiti moto katika hifadhi
• Kukusanya na kutunza vielelezo vya ushahidi na kutoa ushahidi Mahakamani
• Kukusanya takwimu za wanyama na mimea kwenye hifadhi
• Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa zinazoendana na taaluma yake
7.2 SIFA ZA MWOMBAJI
• Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha IV au kidato cha VI wenye Stashahada ya Uhifadhi Wanyamapori (Diploma in Wildlife Management) kutoka Chuo cha Usimamizi Wanyamapori Mweka au Chuo kingine kinachotambuliwa na Serikali.
7.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.
NB: MASHARITI YA JUMLA KWA KAZI ZOTE.
i. Waombaji wote wawe ni Raia wa Tanzania na wenye umri usiozidi miaka 45
ii. Waombaji wote waambatishe cheti cha kuzaliwa.
iii. Waombaji ambao tayari ni watumishi wa Umma na wamejipatia sifa za kuingilia katika kada tofauti na walizonazo, wapitishe barua zao za maombi ya nafasi za kazi kwa waajiri wao na Waajiri wajiridhishe ipasavyo.
iv. Nafasi ya kazi inayoombwa iandikwe juu ya bahasha, kutozingatiwa hili kutasababisha maombi ya kazi kuwa batili.
v. Waombaji waambatishe maelezo binafsi yanayojitosheleza (Detailed C.V) yenye
anwani na namba za simu za kuaminika pamoja na majina ya wadhamini (referees) watatu wa kuaminika.
vi. Maombi yote yaambatane na vyeti vya taaluma, maelezo, nakala za vyeti vya kidato cha nne na kidato cha sita kwa wale waliofikia kiwango hicho na vyeti vya kuhitimu
mafunzo mbalimbali kwa kuzingatia sifa za kazi husika. Viambatanisho hivyo vibanwe sawa sawa kuondoa uwezekano wa kudondoka au kupotea.
- Postgraduate/Degree/Advanced Diploma/Diploma/Certificates.
- Cheti cha mtihani wa kidato cha IV na VI
- Computer Certificate
- Vyeti vya kitaaluma (Professional certificates from respective boards)
- Picha moja "Passport size" ya hivi karibuni iandikwe jina kwa nyuma.
vii. Testmonials", "Provisional Results", "Statement of results", hati matokeo za kidato cha nne na sita (FORM IV AND FORM VI RESULTS SLIPS) HAVITAKUBALIWA.
viii. Waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (TCU na NECTA).
ix. Waombaji waliostaafishwa katika Utumishi wa Umma hawaruhusiwi kuomba isipokuwa kama wanakibali cha Katibu Mkuu Kiongozi.
x. Waombaji kazi ambao tayari ni waajiriwa katika nafasi za kuingilia walioko katika Utumishi wa umma wasiombe na wanatakiwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika Waraka Na CAC. 45/257/01/D/140 wa tarehe 30 Novemba 2010.
xi. Uwasilishaji wa taarifa na sifa za kugushi wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.
xii. Mwisho wa kupokea barua za maombi ni tarehe 18 Januari, 2015
xiii. Aidha, uwasilishaji wa barua kwa mkono katika ofisi za Sekretarieti ya ajira HAURUHUSIWI.
xiv. Maombi yanaweza kuandikwa kwa Lugha ya Kiswahili au Kiingereza na yatumwe kupitia posta kwa anuani ifuatayo.
Katibu, | AU | Secretary, |
Sekretariati ya Ajira katika | | Public Service Recruitment |
Utumishi wa Umma, | | Secretariat, |
SLP.63100, | | P.O.Box 63100 |
Dar es Salaam. | | Dar es Salaam. |
0 comments:
Post a Comment