Wednesday, May 21, 2014

Ban Ki Moon AIPONGEZA TANZANIA KWA ULIPAJI WA MICHANGO YAKE

 
 
 
 
Na Mwandishi Maalum
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, ametoa shukrani na pongezi za pekee kwa kuwa moja ya nchi 29 kati ya 193 ambazo hadi kufikia Mei Sita mwaka huu, zilikuwa zimelipia kwa ukamilifu na kwa wakati michango yake katika Umoja wa Mataifa.
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kati ya nchi hizi ambazo katibu Mkuu amezipongeza. Tanzania imelipa zaidi ya dola za kimarekani 450,000 kama sehemu ya michango yake kwa Chombo hicho cha Kimataifa.
Na kwa miaka mitano mfulululizo imekuwa ikilipa kwa wakati na kwa ukamilifu.
Kwa Tanzania kulipitia michango siyo tu kwamba, ni kielelezo cha uwajibikaji kama nchi mwanachama, lakini pia ni utekelezaji wa utawala bora na ni heshma kwa taifa mbele ya Jumuiya ya Kimataifa.
Pongezi za Ban ki Moon kwa nchi hizo zimo katika taarifa yake kuhusu hali Fedha katika Umoja wa Mataifa.
Taarifa hiyo iliyowasilishwa na kisha kujadiliwa na Wajumbe wa Kamati ya Tano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa inayohusika na masuala ya Utawala na Bajeti ya Umoja wa Mataifa. Katibu Mkuu amezitaka nchi nyingine kuiga mfano wa nchi hizo kwa kile alichosema hali nzuri ya fedha ya Taasisi hiyo ya Kimataifa pamoja na uendeshaji wa shughuli zake, unategemea sana michango ya wanachama wake, michango inayotakiwa kutolewa kwa wakati na kwa ukamilifu.
Kila nchi mwanachama hutakiwa kulipa kiasi cha michango katika bajeti za Umoja wa Mataifa kutokana na uwiano wa uchumi wake katika dunia kama ilivyoainishwa katika Katiba ya Umoja wa Mataifa. Bajeti za Umoja wa Mataifa kwa mwaka ni zaidi ya bilioni 10 zikijumuisha bajeti ya Kawaida, bajeti za misheni za kulinda Amani na mahakama za kimataifa za makosa ya Jinai. Pia kuna bajeti za miradi maalum kama ukarabati wa Jengo la Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kiasi cha dola 2 bilioni kwa mradi wote.
Nchi nyingine ambazo zimekwisha kulipia michango yake ni Australia, Austria, Brunei Darussalam Canada, Denmark, Equatorial Guinea, Finland, Hungary, Germany, Iceland, Israel, Japan, Latvia, Liechtenstein na Netherlands Nyingine ni New Zealand, Norway, Samoa, Senegal, Singapore, Sweden, Switzerland, Timor-Lester, Turkmenistan, , Georgia, Kenya na Jamhuri ya Korea.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mhe. Ban Ki Moon

Related Posts:

  • Programme Manager, Tanzania Programme Manager, Tanzania Reporting to the Country Director, the Programme Manager will provide programmatic support which includes developing and maintaining strategi… Read More
  • Results Programme Manager Results Programme Manager The Results Programme Manager is responsible for leading the development, optimization and utility of the Results Management IT based systems (… Read More
  • East Africa Legal Analyst East Africa Legal Analyst Exceptional professional with 3+ years of experience to oversee One Acre Fund compliance with local laws and be the point person for … Read More
  • Employment Law Analyst Employment Law Analyst Exceptional professional to oversee One Acre Fund compliance with local laws and be the point person for legal research and advisory … Read More
  • East Africa People Operations Associate East Africa People Operations Associate Early-career professionals with 2 – 5+ years work experience to serve in a position that combines both field and management … Read More

0 comments:

Post a Comment