Monday, August 19, 2013

Usaili wa models watakaoshiriki kwenye Ally Ramtullah 2014 Collection





Usaili wa models watakaoshiriki kwenye Ally Ramtullah 2014 Collection
Picture
Picture
Picture
Mwanamitindo maarufu hapa nchini Ally Rehmtullah amefanya maandalizi ya awali ya fashion show yake itayofanyika 30th August mwaka huu katika Hoteli ya Serena ambapo zaidi ya wanamitindo 30 wasichana na wavulana watashiriki katika maonyesho hayo kabambe.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi kwenye mahojiano maalum Rehmtullah amesema kwenye
onesho la mwaka huu wasichana watashiriki 20 na wavulana 10 ambao watavaa mavazi mbalimbali yaliotengezwa na kubuniwa na Rehmtullah mwenyewe kwa kuzingatia mila na desturi za Kiafrika.

Kwenye mchujo huo majaji watano watashiriki kuchagua warembo wenye mvuto, kujiamini na wenye kuwa na muonekano mzuri kwenye jukwaa ili kuwavutia wageni waalikwa ambao watakuwa ni wabunge, mawaziri na viongozi mbalimbali.

Rehmtullah alilisitiza mwaka huu kwamba onyesho la mitindo ya mavazi yatafana baada ya kudhamini wa makampuni kadhaa makubwa hapa nchini.

DSC_0050

Pichani juu na chini ni Models wa kike wakipita mbele ya majaji wakati wa Audition ya kutafuta washiriki watakaonyesha mavazi kwenye Onyesho la Mavazi la Ally Rehmtullah 2014 Collection.
DSC_0053
DSC_0082
Pichani juu na chini ni Models wa kiume wakipita mbele ya majaji kwa ajili ya kuchaguliwa kushiriki kwenye Ally Rehmtullah 2014 Collection Fashion Show.
DSC_0069
DSC_0071



Related Posts:

0 comments:

Post a Comment