Monday, August 26, 2013

Taarifa rasmi ya CCM ya sababu za kumvua uanachama Mansoor Himid (Mb)



Taarifa rasmi ya CCM ya sababu za kumvua uanachama Mansoor Himid (Mb)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyomalizika leo imejadili kwa kina Masuala mbalimbali likiwemo pendekezo la Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Magharibi - Zanzibar la kumvua uanachama Ndugu Mansoor Yussuf Himid, Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi wa Kiembesamaki.

Baadhi ya tuhuma za Ndugu Mansoor Yussuf Himid ni pamoja na:-
  1. Kushindwa kusimamia malengo ya CCM na kutekeleza masharti ya uanachama.
  2. Kushindwa kutekeleza wajibu wa mwanachama na kukiuka Maadili ya Kiongozi wa CCM.
  3. Kuikana Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010-2015 na kuisaliti CCM.

Baada ya kujiridhisha vya kutosha na tuhuma dhidi ya Ndugu Mansoor Yussuf Himid, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) imeridhia uamuzi wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Magharibi Zanzibar wa kumfukuza uanachama. Kwa uamuzi huo wa kumvua uanachama wa CCM Ndugu Mansoor Yussuf Himid, yeye kwa sasa sio Kiongozi tena wa CCM.

Imetolewa na:

Nape Moses Nnauye,
KATIBU WA NEC ITIKADI NA UENEZI CCM TAIFA
26/08/2013



Related Posts:

  • Finance ManagerJob Title : Finance ManagerSource : The Guardian, August 3, 2011Requirements : A Masters Degree in Finance, Management, Economics,Public Accounting/Administration or Certified Public Accounting and 6years of professional expe… Read More
  • Legal Administrative and Personnel OfficerJob Title : Legal Administrative and Personnel OfficerSource : Daily News, August 5, 2011Requirements : Should possess a Degree in Law and Human ResourceManagement or Administration from a recognized University plus atleast t… Read More
  • DriverJob Title : DriverSource : The Guardian, August 5, 2011Requirements : Driving licence "C" plus 2 years experience in the samepost or similar position, preferred in an international NGOJob Description :To dispatch an… Read More
  • AccountantJob Title : AccountantSource : The Guardian, August 5, 2011Requirements : A recognized qualification in financial management and accountingJob Description :To guarantee the record-keeping and the reliabilityof accounts and fi… Read More
  • Neno la leoHere is your word for today:Verse: 1 Peter 3:12For the Lord is watching His children, listening to their prayers.- The eyes of the Lord are watching His children.- God is interested in you and me!- His ears are att… Read More

0 comments:

Post a Comment