Sunday, May 25, 2014

Mkuu wa Tume ya Uchaguzi ya Malawi akaidi Amri ya Rais Joyce Banda ya kufuta matokeo ya uchaguzi.....Asema Rais hana mamlaka ya kuingilia tume ya uchaguzi




Mkuu wa Tume ya Uchaguzi ya Malawi akaidi Amri ya Rais Joyce Banda ya kufuta matokeo ya uchaguzi.....Asema Rais hana mamlaka ya kuingilia tume ya uchaguzi

Mkuu wa Tume ya Uchaguzi ya Malawi Justice Mbendera amekaidi Amri ya Rais Banda ya kufuta matokeo ya uchaguzi. Mbendera amewaagiza maofisa wa tume ya uchaguzi kuendelea na zoezi la kuhesabu kura na kuomba ushirikiano wao wa dhati katika kipindi hiki kigumu.
 
Amesema Rais hana mamlaka ya kuingilia tume ya uchaguzi ambayo inafanya kazi kikatiba na kisheria. Pia Rais Wa chama cha wanasheria wa Malawi (MLS) na Pia Mwanasheria Mkuu wa Zamani wa Malawi wameongea na Vyombo vya Habari Mud Mfupi uliopita na kusema ibara aliyoitaja Rais haimpi mamlaka ya kufuta uchaguzi..

Wamesema kifungu cha 5 cha sheria ya uchaguzi wa Bunge na Rais kinaipa Mamlaka Jukumu lote tume ya uchaguzi kusimamia mchakato wa Uchaguzi. Pia kifungu cha 100 cha sheria hiyo kinatoa haki ya chama au mgombea kulalamika kwa tume kuhusu ukiukwaji wa Mwenendo wa Uchaguzi na kama ndani ya masaa 48 hali hiyo isiporekebishwa kwa kiwango cha kuridhishwa basi kifungu namba 113 cha sheria hiyo hiyo kitatumika kupeleka mashtaka Mahakama Kuu.

Hata hivyo Mwanasheria mkuu akizungumzia Amri hiyo ya Rais leo hii amesema "Kuna Mtu anafanya uhaini hapa sasa" na kuendelea kudai kuwa Rais amefanya uhaini kwa kukiuka ibara ya 88 ya katiba ya nchi kutoa "Presidential Decree" bila sababu yoyote ya msingi inayozingatia katiba na mamlaka ya kisheria 



Source: Jamii forum


Related Posts:

  • Tutorial and Teaching Assistants (30 Positions)Job Title : Tutorial and Teaching Assistants (30 Positions) Source : St. John�s University of Tanzania Requirements : Degree holder in Business Administration, Science with Education, Arts with Education, Information and Co… Read More
  • Neno la leoHere is your word for today:Verse:           Psalm 18:28 You, O Lord, keep my lamp burning; my God turns my darkness into light.- The Lord is the one who sustains you. - God will keep the light of your lamp burning.- Light sp… Read More
  • Assistant Lecturers (40 Positions)Job Title : Assistant Lecturers (40 Positions) Source : St. John�s University of Tanzania Requirements : Masters holder in any of the above named subjects with a GPA of not less than 3.5 in a first degree. Job Description :W… Read More
  • Senior Lecturers (30 Positions) Job Title : Senior Lecturers (30 Positions) Source : St. John�s University of Tanzania Requirements : In Professional Accounting, Finance, Economics, Human Resources and Management, Business Mathematics, Marketing, Healt… Read More
  • International Climate Protection FellowshipsThe International Climate Protection Fellowship Programme for prospective leaders from emerging and developing countries is entering its third round.  Each year, up to twenty International Climate Protection Fellowships are… Read More

0 comments:

Post a Comment