Wednesday, July 18, 2012

Meli yazama Zanzibar

 18 Julai, 2012 - Saa 14:12 GMT

Habari za hivi punde

Meli iliyokuwa imewabeba takriban watu miambili imethibitiswha kuzama katika bahari ya hindi eneo la Chumbe kisiwani Zanzibar. Meli hiyo kwa jina SKAGIT ilikuwa inatoka Dar Es Salam kuelekea Zanzibar.

Kulingana na taarifa za vikosi vya wanamaji , meli hilyo ilianza kupata matatizo baada ya kutokea mawimbi makali.

Jeshi la polisi la wanamaji nchini Tanzania limeanza shughuli za kuwaokoa watu zaidi ya mbia mbili wanaohofiwa kuwa kwenye meli ya Skagit inayoripotiwa kuzama huko visiwani Zanzibar.

Kwa mujibu wa taarifa za polisi, ingawa hawajathibitisha idadi kamili ya abiria waliomo kwenye meli hiyo, lakini wamethibitisha kwamba meli hiyo imepigwa na dharuba ya upepo mkali katika eneo la Chumbe pindi ilipokuwa inatoka jijini Dar es Salaam kuelekea visiwani Zanzibar.

Itakumbukwa kwamba, ni takriban mwaka mmoja sasa tokea ajali ya meli iliyokuwa imezidisha mizigo kuzama katika pwani ya kisiwa cha Zanzibar ikiwa na watu takriban 800.


Source: BBC

Related Posts:

  • PRODUCTION AND MAINTENANCE ENGINEER       PRODUCTION AND MAINTENANCE ENGINEER Qualifications:  Holder of degree in Electrical/Electro/Mechanical or equivalent registered with Engineers registration Board and must have … Read More
  • Rwanda Civil Aviation Authority Vacancies , July 2014   I. BACKGROUND Rwanda  Civil Aviation Authority IRCAA is a 24 hour operational organisation with its headquarters in Kigali. Enjoying Financial and Administrative autonomy, it is charged with … Read More
  • Financial Education Expert   Financial Education Expert Background: Savings Banks foundation for International Cooperation (SBFIC's a German NGO which is promoting the Micro-Finance Sector in Rwanda Financial education is a… Read More
  • Jobs at Olleh Rwanda Networks , July 2014         Olleh Rwanda Networks, Ltd ("oRn Ltd") is a licensed company that has been incorporated under the laws and regulations of the Republic of Rwanda. The company is engaged in the… Read More
  • Commissioner of Quality Assurance Department   (INTERNAL AND EXTERNAL) Rwanda Revenue Authority is a quasi-automous body charged with the task of assessing, collecting, and accounting of Fiscal and Non-Tax Revenues of the Government of Rwanda.… Read More

0 comments:

Post a Comment