Taarifa
iliyoifikia hivi punde toka mkoani Pwani,zinaeleza kuwa
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro kupitia tiketi ya Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Mh. Rejia Mtema amepata ajali mbaya
sana mapema leo asubuhi katika eneo la Ruvu na kufariki dunia papo hapo
wakati akiwa safarini kuelekea Mkoani Morogoro.
Kwa
Mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo walisema kuwa mbunge huyo ambaye
alikuwa akiendesha mwenyewe gari lake amepinduka na gari hilo mara baada
ya kumshinda wakati akijaribu kulipita gari lililokuwa mbele yake
katika eneo hilo la Ruvu.
Ndani
ya Gari hilo kulikuwa kuna watu wengine wanne ambao bado
hawajatambulika ni kina nani na wako kwenye hospitali ya Tumbi Kibaha
mkoani Pwani kwa Matibabu.
tutaendelea kujuzana zaidi kadri taarifa zitakavyokuwa zikitufikia.
Picha kwa hisani ya Michuzi.
0 comments:
Post a Comment