Saturday, October 6, 2012

ICISO KUANZA MIDAHALO JIMBONI KWA PROF MSOLLA LEO



Mbunge wa  Kilolo Prof Peter Msolla ambaye leo anaanza Mdahalo huo
Mbunge wa jimbo la Isimani ambaye pia ni waziri wa nchi ofisi ya  waziri mkuu Sera na uratibu wa bunge Mhe Wiliam Lukuvi ambaye atafuata kwa mdahalo huo tarehe 10 mwezi huu
Mbunge wa jimbo la Iringa mjini Mch Peter Msigwa (chadema) bado zamu yake

Mbunge wa  jimbo la Kalenga ambaye ni waziri wa fedha na uchumi Dkt Wiliam Mgimwa bado muda  wake

WABUNGE mkoani Iringa kukutanishwa na wapiga kura wao katika mdahalo wa kutathimini haki na fursa sawa kwa jinsi zote majimboni mwao.

Katika mdahalo huo ulioandaliwa na mtandao  wa mashirika yasiyo ya kiserikali katika mkoa wa Iringa(ICISO -UMBRELLA) kwa kushirikiana na mitandao ya AZAKI  ya halmashauri ya manispaa ya Iringa (IMUCISO) na Iringa Vijijini (IRUNGO) na wilaya ya Kilolo (KIDINGOU) ,Mbunge wa jimbo la Kilolo Prof. Peter Msolla kuanza Leo katika jimbo lake.

Akizungumza  na waandishi wa habari jana ofisini kwake katibu mtendaji wa ICISO-UMBRELLA Raphael Mtitu alisema kuwa tayari wabunge wa majimbo yote wamepewa barua za ushiriki wao katika midahalo hiyo.


Mititu alisema mbali ya Kuanza Leo katika jimbo la Kilolo midahalo Kama hiyo itafanyika jimbo la Kalenga linaloongozwa na waziri wa fedha na uchumi Dkt Wiliam Mgimwa, jimbo la Iringa mjini linaloongozwa na mchungaji Peter Msigwa na jimbo la Isimani linaloongozwa na waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera ya uratibu wa bunge Wiliam Lukuvi

Alisema kuwa   lengo la mdahalo huo ni kuongeza uewelewa kwa wananchi kuhusu umuhimu wa haki na fursa sawa kwa jinsia katika mkoa wa iringa na wilaya zake kwa ujumla."lengo ni kuwapa wanajamii uelewa juu ya haki za kijinsia na kupunguza matukio ya ubaguzi na unyanyasaji wa kijinsia katika ngazi mbalimbali katika kaya,familia na jamii.

Aidha mdahalo hiyo itakayofanyika tarehe tofauti na ukianza na jimbo la kilolo tarehe 6 mwezi huu katika shule ya sekondari image na kufuatia jimbo la ismani katika ukumbi wa christopher itunundu tarehe 10 ni muendelezo wa mradi wa kuimarisha mahusiano kati ya wananchi na wawakilishi wao ambao unatelekezwa kwa njia ya midahalo.
walengwa wa midahalo hiyo ni wananchi wote na wanaombwa wajitokeze kwa wingi kwa lengo la kupata elimu hiyo ya fursa sawa kwa jinsia zote.
MWISHO

0 comments:

Post a Comment