Wednesday, May 21, 2014

BARABARA KIJICHI - MBAGALA KUU NI HATARI ZAIDI YA HATARI!

 
 
 
 
Barabara ya Kijichi – Mbagala Kuu, ndani ya jiji la Dar es Salaam kama ilivyokutwa jana na Mdau Nathan Mpangala. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Butiama, Bw. Haji Mgaya, alisema, dhahma hiyo ni ya muda mrefu na Manispaa ya Temeke ina taarifa hiyo kwa kupindi chote hivyo,lakini mpaka leo iko kimya tu.
Hapa dereva 'akilala' tu, kilio kitongoji kizima zikifuatiwa na salamu za rambirambi nyiiingi toka kwa viongozi.
Inawezekana Manispaa ya Temeke haina picha halisi ya hatari hii!!!
Halafu hapo hapo ni kituo cha daladala! Manispaa ya Temeke hata alama za hatari pia hakuna?
Kwa maana nyingine gari ikitumbukia hapa, mpaka ije ijikite chini itakuwa imepiga samasoti za kutosha!

0 comments:

Post a Comment